Mwonekano wa gari hilo baada ya kupata ajali….Gari dogo aina ya Toyota RAV4 limepinduka Jumatano Februari 25,2015 katika kijiji cha Mbela wilayani Misungwi, mkoani Mwanza na kujeruhi watu kadhaa waliokuwa ndani yake baada ya kumshinda dereva wake wakati lilikata kona na hivyo kuanguka katika bonde la daraja.
Kwa mujibu wa mashuhuda, gari hilo lenye usajili wa T 358 CBA mali ya Machalo Joseph, lilikuwa likiendeshwa na Festo Kakula wa Misungwi, na baada ya ajali majeruhi walikimbizwa katika hospitali ya Mitindo wilayani Misungwi.


Wasamaria wema wakitoa msaada.



 
Top