Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Habari Ikulu,Salva Rweyemamu amenukuliwa na Redio BBC Swahili akisema kuwa Rais wa Burundi,Pierre Nkurunziza hayupo Tanzania. Akizungumza na BBC Swahili, Rweyemamu amesema kuwa Nkurunziza alishaondoka Tanzania na hivyo Tanzania haina cha kusema juu ya alipo Nkurunziza.
Msemaji wa Nkurunziza amethibitisha kuwa Nkurunziza ameondoka Tanzania. Lakini,amekataa kusema alipo kwa sababu za kiusalama. Msemaji huyo amedai kuwa Rais Nkurunziza bado anadhibiti utawala wa Burundi.
 
Top