Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe kulia na kushoto ni Amos Makalla.

Matokeo ya awali kura za maoni CCM yameonekana kuwa mwiba kwa mawaziri watano pamoja na baadhi wa wabunge kupitia chama hicho kufuatia kuangushwa na kuchaguliwa wengine.

Aliyepata kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utawala Bora na pia Waziri wa Katiba na Sheria akikwama katika mchakato wa kurejea bungeni, naibu wake katika Wizara wa Mambo ya Ndani, Pereira Silima naye ameanguka katika kura za maoni huko jimbo la Bumbwini, Unguja.

Mwanasiasa mwingine aliyekwama katika kura za maoni ni Mahadhi Juma Mahadhi ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa katika Jimbo la Paje, Unguja huku mshindi akiibuka kuwa Jaffar Sanya Jussa.

Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima naye ameripotiwa kuanguka katika kura za maoni katija Jimbo la Mkuranga mkoani Pwani.

Mwingine ni Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dk Milton Makongoro Mahanga ambaye baada ya kuanguka ametimkia Chadema.

Kutoka Jimbo la Mvomero mkoani Morogoro, aliyewahi kuwa mbunge wa zamani wa jimbo hilo, Suleiman Saddiq `Murad’ amefanikiwa kumwangusha mshindani wake wa siku nyingi, Amos Makalla ambaye alilitwaa jimbo hilo mwaka 2010.

Nalo Jimbo la Uzini ambako mwanasiasa nguli aliyepata kuwa waziri katika wizara mbalimbali za Serikali ya Muungano, Muhammed Seif Khatib ameshindwa katika kura za maoni.

Kwa upande wa wabunge nao wamekuwa na wakati mgumu majimboni kwao, akiwemo Ismail Aden Rage wa Tabora. Mbunge mwingine aliyeshindwa katika kura za maoni ni Mtutura Abdalla wa Tunduru Kusini.

Credit:Malunde1 Blog
 
Top