Mbunge wa Jimbo la Ngara mkoani Kagera Mhe.Alex R.Gashaza akikagua ujenzi wa Vyumba vya Madarasa,Mabweni na Matundu ya Vyoo katika Shule ya Sekondari Murusagamba.

Mbunge wa jimbo la Ngara mkoani Kagera Mhe.Alex Gashaza ametoa shilingi milioni 2 za mfuko wa jimbo hilo kukiwezesha Kikundi cha walemavu kata ya Rulenge wilayani humo kuendeleza miradi yao.


Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Ngara anayesimamia tarafa ya Rulenge na Murusagamba Bw Lengo Kapfusi amesema kikundi hicho kinajihusisha na Ufugaji wa Mbuzi na upandaji wa Miti pamoja na kilimo cha Bustani. 


Bw Kapfusi amesema mfuko huo pia umetoa shilingi milioni 4 kuunga mkono Juhudi za Wananchi wanaojenga vyumba vya Madarasa katika shule ya msingi Rulenge na Mubwilindebaada ya wanajamii wa maeneo hayo kuchangia nguvu zao.


Amewataka walengwa waliopatiwa fedha hizo kuzitumia kwa malengo yaliyokusudiwa ili kupata Tija katika Maendeleo endelevu.

Aidha Mwenyekiti wa kikundi cha walemavu Rulenge Bw Charles Kagambokabi amekiri kupokea fedha hizo na kwamba zimetumika kununua mbuzi 11 na fedha nyingine zimeelekezwa kwenye shughuli za ujasiriamali na kukopeshana.
 
Top