Dereva
huyo alikuwa safarini jana tarehe 18/10/2014 akitokea Dar Es salaam kuchukua
gari hiyo bandarini kuelekea Bujumbura nchini Burundi. Aidha inasemekana kwamba
baada ya kufika eneo hilo la Kabanga garden hotel alipaki gari yake vizuri na kisha
kuomba kwanza kwenda haja kujisadia kabla hajaandikisha chumba.
Umati wa watu ukimiminika kushuhudia tukio hilo |
Mwili
wake umegundulika leo tarehe 19/10/2014 asubuhi na mtu aliyekuwa anaingia
chooni humo kujisaidia. Jeshi la polisi la kituo cha Kabanga limefika eneo la
tukio na kuthibitisha tukio hilo. Aidha vipimo vya daktari vimeonesha kuwa
marehemu alikuwa mgonjwa hivyo ugonjwa huo ambao haukutajwa mara moja ndio
umepelekea umauti huo ulomfika.
Gari mpya ya IT alokuwa nayo marehemu |