
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kagera, Henry Mwaibambe alisema wanandoa hao walikuwa na ugomvi wa muda mrefu.
Inadaiwa baada ya kujibizana kwa maneno, mume alimkata mkewe sehemu za mdomo na mkono wake wa kulia.
Kamanda Mwaibambe alisema mume aliingia ndani ya nyumba yake na kuchukua gauni la mkewe na kujining’iniza darini katika sebuleni ya nyumba yake.
Mwaibambe alisema Velidiana amelazwa katika Hospitali ya Ndolage wilayani Muleba na hali yake inaendelea vizuri.
Mwili wa marehemu ulichukuliwa na ndugu zake na kuzikwa baada ya uchunguzi kukamilika.
BONYEZA HAPA NA LIKE KUJIUNGA NASI FACEBOOK