Zaidi ya watu 40 wamenusurika kifo huku mmoja akikatika viungo vya miguu na wengine kujeruhika vibaya baada ya lori moja lilionekana kuwa ni la jeshi kugongana uso kwa uso na gari la abiria aina ya COSTA la Ubungo -Tegeta eneo la Tegeta jijini Dar es salaam.Tukio hilo limevuta hisia za mamia ya wakazi wa Tegeta huku baadhi ya mafundi gereji wa Tegeta wakijaribu kutumia vifaa maalumu kukata mabati ya magari kwa nia ya kunasua baadhi ya majeruhi walionasa ndani ya COASTA hiyo kusuru abiria walioonekana kunasa katika vyuma vya magari hayo.

Baadhi ya mashuhuda na dereva wa COSTA pamoja na kuomba eneo la kibaoni kuweka njia ya mzunguko maarufu kama ROUND ABOUT kwa lengo la kuepusha madereva wanao lazimika kugeuza kwa dharura katika njia kuu maarufu kama UTAN kutokana na njia hiyo kukosa fursa ya kugeuza endapo kuna ulazima wa kufanya hivyo.

Pia wamemtupia lawama Dereva wa Lori kama msababisha ajali kwa kukosa hekima ya kuchukua tahadhari kabla ya kufanya hivyo.

Kamanda wa polisi mkoa kipolisi Kinondoni Kamilius Wambura amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo akieleza kutoa taarifa mara baada ya uchunguzi kufanyika.
Via>>ITV 

 
Top