Mgombea Ubunge wa Jimbo la Ngara mkoani kagera kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, Dr Petter Bujari akiwahutubia Wananchi wa Ngara mjini wakati wa mkutano wa Kampeni uliofanyika September 06,2015 kwenye uwanja wa Posta ya zamani.
Akizungumza katika mkutano huo wa Kampeni katika Kata ya Ngara mjini,Dr Bujari amesema kuwa akipewa ridhaa ya Kuwa Mbunge wa Jimbo la Ngara ,atahakikisha anashirikiana na Wananchi wa Ngara kutumia fursa zinazowazunguka Kuongeza kipato chao, Kusimamia utawala wa sheria na haki, Kutatua kero na matatizo hasa ya wafanyakazi , walimu na madaktari aliobainisha kuwa na kero kubwa ya kunyimwa haki zao pamoja na kuondoa kero za wafugaji na wakulima na kupanua na kukuza kilimo na ufugaji.

Dr Bujari amesema Wanangara wanapaswa kuwa Wazalendo kwa taifa lao kwa kufanya maamuzi sahihi kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba 25 mwaka huu 2015 kwa kuchagua viongozi wenye sifa watakaochochea maendeleo ya Ngara na taifa kwa ujumla.




Mwananchi wakimsikiliza Mgombea Ubunge wa Jimbo la Ngara mkoani kagera kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, Dr Petter Bujari katika mkutano huo wa Kampeni katika Kata ya Ngara mjini.




 
Top